Ni Wewe Kiswahili Poem


Nakutuliza moyoni
Ulinipenda na roho yako yote
Ukanipa mahaba ya kutosha
Ambayo yaniloweza hadi sitamani yaishe
Penzi lako latuliza mawazo yangu
Mvua ikinyesha
Giza likiingia mawinguni
Unawasha taa na pendo lako
Na kufukuza upweke
Busu lako no tamu
Tamu zaidi ya tunda lolote duniani
Nakutaka
Nakuhitaji
Nipe ruhusa yako
Nikuweke moyoni milele
Dhahabu haiwezi kulinganisha
Jinsi tunavyopendana
Hata ukame uwepo, theluji inyeshe
Mimi na wewe ni hisia moja

No comments

Post a Comment

© Chaotic Soul of a Poet
Maira Gall